Michelle
Obama (wa pili kushoto) anaonekana hana raha wakati akiwa Saudi Arabia
na mumewe, Rais Obama, wakati walipokwenda kuomboleza msiba wa Mfalme
Abdullah.
Thursday, January 29, 2015
Monday, January 26, 2015
3:32 AM
Hon.Cisko
Thursday, January 22, 2015
5:44 AM
Hon.Cisko
Msimamizi
wa bodi ya michezo ya kubahatisha,Mrisho Millao(kulia)akiandika namba
ya Hynes Petro Kanumba (20) Mkazi wa kijiji cha Inyonga mkoani Rukwa
aliyeibuka mshindi wa Shilingi Milioni 10/- katika droo ya nane kupitia
promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,wengine
katika picha kutoka kushoto Meneja Uhusiano wa Umma wa kampuni
hiyo,Matina Nkurlu na Meneja uhakiki wa mapato Vodacom Zakaria
Kamweru.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda
15544.
Thursday, January 15, 2015
Tuesday, January 13, 2015
Friday, January 9, 2015
5:13 AM
Hon.Cisko
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Bi. Anne Rose Nyamubi mara
baada ya kuwasili ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo kabla ya
kuelekea kwenye kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum wakiwemo
walemavu wa ngozi cha Buhangija Jumuishi kilichopo mkoani Shinyanga.
Na mwandishi wetu, ShinyangaMKUU wa wilaya ya Shinyanga AnneRose Nyamubi ameomba jamii ya watanzania kusaidia kupatikana kwa zahanati katika kituo cha kulelea watoto walemavu cha Buhangija ili kupunguza adha wanazopata watoto hao katika huduma za afya.
Kauli hiyo ameitoa katika mazungumzo na mwandishi wa habari hizi ambaye alifika katika kituo hicho akiambatana na ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliokuwa ukiongozwa na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Nyamubi amesema kwamba ingawa hospitali ya mkoa ina dirisha kwa ajili ya matibabu ya watoto hao,wakati mwingine inakuwa shida daktari maalumu anayehusika anapokuwa hayupo.
Aidha alisema kwa namna watoto hao walivyo wanahitaji huduma ya karibu ya kitiba ambayo inawezekana kama kituo hicho kingekuwa na zahanati yake.
5:05 AM
Hon.Cisko
Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw.
Ephraimu Kwesigabo akitoa taarifa ya kupungua kwa mfumuko wa bei nchini
kwa mwezi Desemba, 2014 leo jijini Dar es salaam.Wengine ni Meneja wa
Takwimu za Ajira na Bei wa Ofisi hiyo Bi. Ruth Minja (kushoto) na
Johnson Nyella, Meneja Utafiti wa Uchumi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT).
5:00 AM
Hon.Cisko
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai, wakiwa katika Sala na Dua ya kumuombea aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Bibi Fatma Othman Ali kabla ya mazishi yake iliyofanyika Januari 08,2015 katika msikiti wa Mohammed Ali Jang’ombe Zanzibar.
Wednesday, January 7, 2015
3:59 AM
Hon.Cisko
Katibu
wa Jumuiya ya Wafanyakazi wastaafu Pemba Bwana Majid Moh’d akimkabidhi
risala Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwenye
hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Jumuiya hiyo hapo ukumbi wa
Tasaf Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Chake chake Pemba.
3:50 AM
Hon.Cisko
SERIKALI imeombwa kuhakikisha inakomesha ubabe unaotumika kukeketa mabinti wa koo za Kikuria nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha kupambana na ukeketaji cha Masanga, Tarime Sista Germaine Baibika akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji.
Alisema jumla ya mabinti 634 wamehitimu mafunzo ya miezi miwili yanayogusa haki za binadamu, haki zao, masuala ya afya na kuzitambua na kuezinzi mila nzuri.
Aidha wamejifunza kazi za sanaa na usanii.
Alisema adha kubwa wanayokumbana nayo mabinti hao waliotoka katika kituo hicho ni kukamatwa kwa nguvu na kupitishwa kisu cha Ngariba bila wao wenyewe kuafiki kwa dai la kuendeleza mila.
“Hii sio mila” anasema sista Germaine na kuongeza kuwa hakuna mila inayotengenezwa kunyanyasa watu wengine au kulazimisha mambo yasiyofaa katika jamii, mila hiyo ikiwepo lazima ipigwe vita.
Monday, January 5, 2015
11:20 PM
Hon.Cisko
Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akionyesha picha za viongozi wa Panya Road kwa wanahabari.
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,
linawashikilia watu 510 wakiwemo viongozi watatu wa kundi
linalojihusisha na uhalifu la ‘Panya Road’ .Watu hao wamekamatwa katika operesheni inayoendeshwa na jeshi hilo, kupambana na uhalifu.
11:12 PM
Hon.Cisko
MWALIMU Gaudencia Gitano (40) anayefundisha Shule ya Msingi Kivelu jijini Dar es Salaam, amedai huenda yeye ndiye anayeongoza kwa kupigwa kuliko wanawake wengine wote jijini, baada ya kudai anazo RB tano za vipigo tofauti kutoka kwa mumewe kwa nyakati mbalimbali tangu aolewe Oktoba 25, 2002, katika ndoa ya kiserikali iliyofungwa Ilala Boma.
11:07 PM
Hon.Cisko
MTANGAZAJI wa runinga Maimartha Jesse, ameweka wazi kuwa pamoja na watu kulalamika kuwa mwaka uliopita ulikuwa mgumu kifedha kwa upande wake amefanikisha kuingiza kiasi cha shilingi milioni 28 ambazo amezipata kupitia kazi zake za kila siku ikiwemo ya kundi lake maarufu la Baikoko.
Sunday, January 4, 2015
10:09 PM
Hon.Cisko
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Uteuzi wa Bwana Masaju ulianza jana, Ijumaa, Januari 2, 2015 na ataapishwa keshokutwa, Jumatatu, Januari 5, 2015, Ikulu, Dar Es Salaam.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Masaju alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bwana Masaju pia amepata kuwa Mshauri wa Sheria wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
3 Januari, 2015
10:06 PM
Hon.Cisko
Kuanzia Mwezi Julai mwaka 2014 mpaka Desemba, bei ya mafuta ghafi imekuwa ikishuka kutoka $110 kwa pipa mpaka $56 kwa pipa. Mporomoko huu wa bei wa zaidi ya 40% haujaleta unafuu kwa mtumiaji wa kawaida wa mafuta ikiwemo wenye daladala na kupelekea nauli za usafiri wa umma kupungua.
Leo bado bei ya mafuta kwenye vituo vya mafuta ni tshs 2029 kwa Petroli na 1909 kwa dizeli, bei ambayo ni karibia ile ile kwa miezi michache iliyopita.
9:46 PM
Hon.Cisko
ACHENI jamani! Vurugu tuzisikie tu kwa wenzetu! Kitendo cha vijana wachache wasio na maadili wanaojiita Panya Road kufanya fujo kidogo katika baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar, wakazi wa jiji hilo wamekitafsiri kitendo hicho na kusema Dar sasa si sehemu salama tena ya kuishi, Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili.
9:39 PM
Hon.Cisko
LICHA ya kushauriwa na daktari kuhusu kutulia na kutovaa viatu virefu kutokana na ujauzito, mwigizaji Aunt Ezekiel ameonekana kuwa ni sikio la kufa kwani ameendelea kuvaa kama kawaida.Aunt aliendeleza ubishi huo Jumatano iliyopita mjini Dodoma alipokuwa amekwenda katika Pati ya Good Bye 2014 iliyoandaliwa na Kampuni ya Endless Fame ambapo mashabiki walimshuhudia Aunt akiwa amevaa kigauni kifupi pamoja na viatu virefu kama kawa.
9:37 PM
Hon.Cisko
Staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akipozi.
Kumekuwa na maneno mengi juu ya nani mzuri kati ya staa wa Uganda,
Zarinah Hassan ‘Zari’ au ‘The Boss Lady’ na Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Wema ametembea na Diamond na sasa Zari anadaiwa kuchukua uskani. Ijumaa
Wikienda limechukua jukumu la kumaliza ubishi ambapo lilibandika swali
hilo kwenye mitandao ya kijamii ya Instagram, Facebook na Twitter.
Maelfu ya mashabiki wao walipata nafasi ya kutoa ya moyoni. Majibu
yaliyopatikana pima mwenyewe, ujiongeze.
Subscribe to:
Comments (Atom)
RSS Feed
Twitter

