Showing posts with label stars. Show all posts
Showing posts with label stars. Show all posts
Monday, April 13, 2015
Thursday, February 5, 2015
2:50 AM
Hon.Cisko

SIKU chache baada ya Nasibu Abdul ‘Diamond’ kuweka picha zinazomuonesha mpenzi wake wa sasa Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na kitumbo kinachoashiria kukua kwa ujauzito, mama mzazi wa zilipendwa wa Diamond, Wema Sepetu ‘Madam’, Mariam Sepetu amefunguka kuwa amefurahia tukio hilo.
Wednesday, January 7, 2015
Monday, January 5, 2015
11:07 PM
Hon.Cisko

MTANGAZAJI wa runinga Maimartha Jesse, ameweka wazi kuwa pamoja na watu kulalamika kuwa mwaka uliopita ulikuwa mgumu kifedha kwa upande wake amefanikisha kuingiza kiasi cha shilingi milioni 28 ambazo amezipata kupitia kazi zake za kila siku ikiwemo ya kundi lake maarufu la Baikoko.
Sunday, January 4, 2015
9:39 PM
Hon.Cisko
LICHA ya kushauriwa na daktari kuhusu kutulia na kutovaa viatu virefu kutokana na ujauzito, mwigizaji Aunt Ezekiel ameonekana kuwa ni sikio la kufa kwani ameendelea kuvaa kama kawaida.Aunt aliendeleza ubishi huo Jumatano iliyopita mjini Dodoma alipokuwa amekwenda katika Pati ya Good Bye 2014 iliyoandaliwa na Kampuni ya Endless Fame ambapo mashabiki walimshuhudia Aunt akiwa amevaa kigauni kifupi pamoja na viatu virefu kama kawa.
9:37 PM
Hon.Cisko

Staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akipozi.
Kumekuwa na maneno mengi juu ya nani mzuri kati ya staa wa Uganda,
Zarinah Hassan ‘Zari’ au ‘The Boss Lady’ na Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Wema ametembea na Diamond na sasa Zari anadaiwa kuchukua uskani. Ijumaa
Wikienda limechukua jukumu la kumaliza ubishi ambapo lilibandika swali
hilo kwenye mitandao ya kijamii ya Instagram, Facebook na Twitter.
Maelfu ya mashabiki wao walipata nafasi ya kutoa ya moyoni. Majibu
yaliyopatikana pima mwenyewe, ujiongeze.Tuesday, December 30, 2014
Tuesday, December 23, 2014
9:35 PM
Hon.Cisko

KIFO cha utata cha mnenguaji nyota Bongo, Mwanaisha Mbegu maarufu kama Aisha Madinda, kimemuibua Suzan Chubwa ‘Queen Suzy’ wa FM Academia, aliyewataka wenzake kuwa makini ili kutojiingiza katika utumiaji wa madawa ya kulevya.
Akistorisha na paparazi wetu, Queen Suzy alisema ameumizwa sana na kifo hicho kwani ameacha pengo kubwa kutokana na unenguaji wake mzuri, huku chanzo cha kifo chake kikiwa hakifahamiki sawasawa.
“Nawasihi wanenguaji wenzangu na wanamuziki wote, tusidanganyike kuingia kwenye vishawishi vya matumizi ya madawa ya kulevya, maana mfano Aisha alikuwa mzuri kweli kwenye kazi, lakini alipojiingiza kwenye unga kiwango chake kikashuka sana,” alisema Queen Suzy.
9:32 PM
Hon.Cisko

MASTAA wa filamu Bongo, Nisha, Odama na Aunt Ezekiel wameipongeza kampuni ya Steps Entertainments kwa kitendo chake cha kuagiza mtambo wa kurekodia filamu kitu ambacho kitawasaidia wasanii kufaidika.
“Kitendo cha kurekodia nje ya nchi kilikuwa kinawafanya wasambazaji kuongeza gharama za filamu zetu kwa walaji, kitu ambacho kilikuwa kikiwafanya wanakimbilia kwa wezi wa kazi zetu kwa sababu ya urahisi wa bei, lakini wao kwa kuleta mtambo huo, ina maana filamu zitashuka bei na zikiwa na ubora, ni jambo zuri sana,” alisema Odama akiwa pamoja na wenzake hao.
Monday, December 22, 2014
9:51 PM
Hon.Cisko

WIKI iliyopita tuliishia pale ambapo staa wa Bongo Fleva, Diamond aliachia video yake ya Number One katika uzinduzi usiyo na kiingilio alioufanya ndani ya Hoteli ya Serena jijini Dar ambapo pia alimzawadia gari, aliyekuwa mwanamuziki nguli nchini, marehemu Muhidin Maalim Gurumo.
Wiki hii tunaendelea ambapo katika kuanika maisha yake, Diamond anasema:
Sunday, December 21, 2014
9:45 PM
Hon.Cisko

STAA wa filamu za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amesema anakumbuka fadhila za marehemu Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’ ndiyo maana amejitoa kwa hali na mali katika msiba wake kwani anawaonea huruma watoto wake ambao aliishi nao kama kaka yao enzi za marehemu alipokuwa na uhusiano na mdau wa Muziki wa Dansi Bongo, Fikiri Madinda.
9:37 PM
Hon.Cisko

WAKATI kila mtu akiamini mwalimu wake wa lugha ya Kiingereza ni Wema Sepetu ‘Madam’ staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibuka na kudai aliyemfundisha lugha hiyo ni aliyekuwa mpenzi wake, Peniel Mungilwa‘Diamond aliwataka watu wote waliokuwa wakiamini Wema ndiye mwalimu wake wa ung’eng’e wafute imani hiyo kwani Penny ndiye mpango mzima.
Thursday, December 18, 2014
8:22 PM
Hon.Cisko

Ijumaa: Umekuwa ukitajwa kuwa wewe ni msanii wa kike unayeongoza kwa kubadilisha mabwana kila kukicha, hili likoje?
Baby Madaha: Ukweli hiyo huwa inatokea tu na huwa sipendi kusumbuliwa na mwanaume, nikiona ananizingua nammwaga. Hata hivyo, kwa sasa nimeamua kutulia kwanza, nafanya kazi, mapenzi pembeni.
Ijumaa: Unadhani kwa nini umekuwa ukiingia kwenye uhusiano kisha kutoswa, ni umachepele wako au kitu gani?
Subscribe to:
Posts (Atom)
RSS Feed
Twitter








