Showing posts with label company. Show all posts
Showing posts with label company. Show all posts

Thursday, December 18, 2014


Mtoto Raphael Barnaba (4) kutoka mkoani Mbeya anayetibiwa miguu katika hospitali ya CCBRT iliyopo jijini Dar es Salaam, akipokea kwa furaha zawadi ya matunda kutoka kwa mfanyakazi wa kampuni ya simu ya Vodacom kitengo cha Rasilimali Watu, Alice Lewis (katikati) wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipotembelea wagonjwa katika hospitali hiyo na kuwagawia matunda kama sehemu ya kampeni ya Pamoja na Vodacom chini ya Vodacom Foundation wakati wa kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka. Akitazama ni mama wa mtoto huyo (wa kwanza kushoto).

Sunday, November 23, 2014


MWISHONI mwa wiki kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania iliibuka kinara wa pili kwa walipa kodi wakubwa na inaongoza katika kundi la sekta ya mawasiliano nchini ambapo haijawahi kutokea.
Akiongea katika kilele cha maadhimisho ya 8 ya Wiki ya Mlipa Kodi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere, Mkurugenzi wa Kitengo cha Elimu ya walipa kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania,Richard Kayombo, aliyataja makampuni 3 yanayoongoza kwa kufuata kanuni bora za ulipaji kodi na utunzaji wa kumbukumbu za kulipa kodi nchini kuwa ni Kampuni ya Bia Tanzania, Kampuni ya Vodacom na Kampuni ya kutengeneza sigara.
Akiongea muda mfupi baada ya kutunukiwa kikombe na cheti cha ushindi kutoka kwa mgeni wa heshima ambaye alikuwa ni Waziri Kiongozi mstaafu wa Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Kelvin Twisa alisema “Napenda kuishukuru Serikali kwa kutambua mchango wetu wa kuchangia mapato na vilevile nawashukuru wafanyakazi wote wa Vodacom na wateja wote ambao wanaendelea kutuweka mbele kwa ushirikiano wao na kutuamini ambapo tumeweza kuwa wachangiaji wakubwa.

Monday, November 17, 2014


Starting a business

Design by hons.CISKO | Blogger Theme by CISKO