Friday, February 20, 2015


Kikundi cha wasanii mkoani Dodoma, kikitoa burudani kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa nne wa wanachama na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, mjini Dodoma. Mkutano huo umemalizika leo Alhamisi Feb 19, 2015

Kaimu mkurugenzi wa fedha na utawala wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Yahaya Ally, akitoa taarifa ya fedha ya Mfuko huo wakati wa mkutano wa nne wa wanachama na wadau wa PSPF, mjini Dodoma. Mkutano huo ulioanza Februari 18, umefungwa leo Alhamisi Februari 19, 2015
 
Baadhi ya washiriki wa mkutano mkuu wa nne wa wanachama na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, wakifuatilia mkutano huo leo, wakati wa ufungaji
Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Gabriel Silayo, akitoa mada kuhusu uwekezaji katika sekta mbalimbali uliofanywa na Mfuko huo, wakati wa mkutano mkuu wa nne wa wanachama na wadau wa PSPF mjini Dodoma. Mkutano huo umemalizika leo Alhamisi Februari 15, 2015  
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, 
Neema Muro, akitoa mada kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko huo kwa wanachama wake, wakati wa mkutano mkuu wa nne wa wanachama na wadau mjini Dodoma
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya mkutano mkuu wa nne wa Wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, wakiongozwa na Meneja wa Masoko na Mawasiliano wa Mfuko huo, Costantina Martin (wapili kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufanikisha mkutano huo kwa mafanikio makubwa. Mkutano huo umemalizika jana Alhamisi Februari 19, 2015
 
 

0 comments:

Post a Comment

Design by hons.CISKO | Blogger Theme by CISKO