
Katibu
wa Jumuiya ya Wafanyakazi wastaafu Pemba Bwana Majid Moh’d akimkabidhi
risala Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwenye
hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Jumuiya hiyo hapo ukumbi wa
Tasaf Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Chake chake Pemba.


Wastaafu
wa Taasisi za Umma za Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na
zile za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanapaswa kushirikiana kwa
karibu katika kutumia ujuzi na Taaluma zao za muda mrefu ndani ya
Jumuiya wanazozianzisha baada ya kustaafu kwao ili waendelee kuchangia
Maendeleo ya Taifa.
Kauli hiyo
imetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
wakati akiizindua rasmi Bodi ya wadhamini ya Jumuiya ya Wastaafu Pemba
hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Tasaf uliopo katika Majengo ya
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar yaliyopo Chake chake Pemba.
Balozi Seif
alisema mashirikiano hayo yatatoa nafasi nzuri kwa wastaafu hao kuondoa
shaka ya kuendeleza maisha yao kwani baadhi yao hupata wakati mgumu
kabla na baada ya kustaafu kwa vile wanakuwa bado hawajajipanga.
0 comments:
Post a Comment