
STAA wa filamu za kibongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ ambaye aliripotiwa kuondoka katika kundi maarufu la Bongo Movie Unity, anadaiwa kutaka kurejea kundini baada ya kuona anakosa madili.
Lakini nyota huyo alipozungumza na gazeti hili, alishangazwa na habari hizo na kudai kuwa anasikia juu ya suala hilo, lakini siyo kweli, kwani pamoja na ukweli kwamba yeye aligombana na mtu mmoja tu Bongo Movie, bado hawezi kutaka kurudi kwa vile yeye kama mjasiriamali, ana vitu vingi vya kufanya.
0 comments:
Post a Comment