
NATISHA! Uhaba mkubwa wa madawa, ongezeko la ada ya kitanda na chakula katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, umesababisha watu wengi kupoteza maisha kufuatia wagonjwa kukosa huduma na hivyo kurejea majumbani mwao.

Baadhi ya wagonjwa wakiwa katika moja ya wodi za Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa baada ya Bohari Kuu ya Madawa (MSD) kusitisha kutoa dawa kwa hospitali hiyo kubwa ya serikali kufuatia deni kubwa, wagonjwa hasa wenye uwezo mdogo wamelazimika kuingia mitaani na kuombaomba kwa wasamaria wema ili waweze kunusuru hali zao.
Katika wodi ya wagonjwa wa moyo,
walilalamikia bei kubwa ya matibabu inayowafanya wasio na uwezo na wasio
na ndugu kuishi kwa kubahatisha. “Hali ni mbaya sana hapa, jana
nimeshuhudia wagonjwa wenzetu wawili wanapoteza maisha kwa sababu
hawahudumiwa tokea majuzi kwa vile hakuna dawa, na tunasikia hata huko
katika mawodi mengine hali ni ya hatari kabisa,” alisema mgonjwa mmoja
aliyeomba hifadhi ya jina lake.
0 comments:
Post a Comment