Monday, April 13, 2015
Friday, April 10, 2015
Tuesday, March 24, 2015
Monday, March 16, 2015
Wednesday, March 11, 2015



Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akisalimiana na Balozi wa China Nchini Tanzania Dr.Lu Youqing alipofika
Ikulu Mjini Zanzibar (kulia) Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi
Zanzibar Xie Yunliang.


Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akifuatana na mgeni wake Balozi wa China Nchini Tanzania Dr.Lu Youqing
baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika alipofika Ikulu Mjini
Zanzibar.[Picha na Ikulu.]
Friday, February 20, 2015



MWAKILISHI
Mkazi wa Shirika la JICA nchini Tanzania, Onishi Yasunora
akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi
Felchesm Mramba (kulia) wakati wa mkutano na waandishi wa kuzungumzia
maendeleo ya miradi ya kuboresha na kukarabati miundombinu ya umeme hapa
nchini. Mkutno huo ulifanyika Dar es Salaam. Pamoja nao ni Waziri pia
mkuu wa Kazi wa Ubalozi wa Japan hapa Nchini, Kazuyoshi Matsunaga.
Friday, February 13, 2015


Ujumbe
wa Kamati ya Bunge ya Ardhi , Maliasili na Mazingira ukiongozwa na
Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Abdulkarim Esmail Hassan Shah (Mafia),
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki na
kuambatana na uongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakisikiliza maelezo
kutoka kwa Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Tumaini Thika
jana. Kamati hiyo iko katika ziara ya mafunzo nchini humo.
Wednesday, February 11, 2015



Mkurugenzi
wa masoko wa Airtel bw. Levi Nyakundi (kushoto) akimkabidhi mmoja kati
ya washindi wa promosheni ya Yatosha Zaidi bi. Mwajabu Omary leo katika
makabidhiano yaliyofanyika katika ofisi za makao makuu ya Airtel
Tanzania. Anayeshuhudia (katikati) Mkurugenzi wa wa kitengo cha
Mawasiliano bi Beatrice Singano Mallaya .Airtel imekabidhi magari matatu
katika hafla hiyo.
Tuesday, February 10, 2015



KIMENUKA!
Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ amemporomoshea matusi mazito
shemeji wa Zarina Hassan ‘Zari’, King Lauwrance akidai amemuudhi sana
kwa kitendo cha kuvujisha picha inayomuonesha akiponda raha nchini
Afrika Kusini ‘Sauz’ na mume wa Zari, Ivan Semwanga, Risasi Mchanganyiko
linakupa mchapo kamili.
Thursday, February 5, 2015



SIKU chache baada ya Nasibu Abdul ‘Diamond’ kuweka picha zinazomuonesha mpenzi wake wa sasa Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na kitumbo kinachoashiria kukua kwa ujauzito, mama mzazi wa zilipendwa wa Diamond, Wema Sepetu ‘Madam’, Mariam Sepetu amefunguka kuwa amefurahia tukio hilo.
Thursday, January 29, 2015
Monday, January 26, 2015


Thursday, January 22, 2015



Msimamizi
wa bodi ya michezo ya kubahatisha,Mrisho Millao(kulia)akiandika namba
ya Hynes Petro Kanumba (20) Mkazi wa kijiji cha Inyonga mkoani Rukwa
aliyeibuka mshindi wa Shilingi Milioni 10/- katika droo ya nane kupitia
promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,wengine
katika picha kutoka kushoto Meneja Uhusiano wa Umma wa kampuni
hiyo,Matina Nkurlu na Meneja uhakiki wa mapato Vodacom Zakaria
Kamweru.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda
15544.
Thursday, January 15, 2015
Tuesday, January 13, 2015
Friday, January 9, 2015



Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Bi. Anne Rose Nyamubi mara
baada ya kuwasili ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo kabla ya
kuelekea kwenye kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum wakiwemo
walemavu wa ngozi cha Buhangija Jumuishi kilichopo mkoani Shinyanga.
Na mwandishi wetu, ShinyangaMKUU wa wilaya ya Shinyanga AnneRose Nyamubi ameomba jamii ya watanzania kusaidia kupatikana kwa zahanati katika kituo cha kulelea watoto walemavu cha Buhangija ili kupunguza adha wanazopata watoto hao katika huduma za afya.
Kauli hiyo ameitoa katika mazungumzo na mwandishi wa habari hizi ambaye alifika katika kituo hicho akiambatana na ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliokuwa ukiongozwa na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Nyamubi amesema kwamba ingawa hospitali ya mkoa ina dirisha kwa ajili ya matibabu ya watoto hao,wakati mwingine inakuwa shida daktari maalumu anayehusika anapokuwa hayupo.
Aidha alisema kwa namna watoto hao walivyo wanahitaji huduma ya karibu ya kitiba ambayo inawezekana kama kituo hicho kingekuwa na zahanati yake.



Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw.
Ephraimu Kwesigabo akitoa taarifa ya kupungua kwa mfumuko wa bei nchini
kwa mwezi Desemba, 2014 leo jijini Dar es salaam.Wengine ni Meneja wa
Takwimu za Ajira na Bei wa Ofisi hiyo Bi. Ruth Minja (kushoto) na
Johnson Nyella, Meneja Utafiti wa Uchumi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT).


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai, wakiwa katika Sala na Dua ya kumuombea aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Bibi Fatma Othman Ali kabla ya mazishi yake iliyofanyika Januari 08,2015 katika msikiti wa Mohammed Ali Jang’ombe Zanzibar.
Wednesday, January 7, 2015



Katibu
wa Jumuiya ya Wafanyakazi wastaafu Pemba Bwana Majid Moh’d akimkabidhi
risala Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwenye
hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Jumuiya hiyo hapo ukumbi wa
Tasaf Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Chake chake Pemba.



SERIKALI imeombwa kuhakikisha inakomesha ubabe unaotumika kukeketa mabinti wa koo za Kikuria nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha kupambana na ukeketaji cha Masanga, Tarime Sista Germaine Baibika akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji.
Alisema jumla ya mabinti 634 wamehitimu mafunzo ya miezi miwili yanayogusa haki za binadamu, haki zao, masuala ya afya na kuzitambua na kuezinzi mila nzuri.
Aidha wamejifunza kazi za sanaa na usanii.
Alisema adha kubwa wanayokumbana nayo mabinti hao waliotoka katika kituo hicho ni kukamatwa kwa nguvu na kupitishwa kisu cha Ngariba bila wao wenyewe kuafiki kwa dai la kuendeleza mila.
“Hii sio mila” anasema sista Germaine na kuongeza kuwa hakuna mila inayotengenezwa kunyanyasa watu wengine au kulazimisha mambo yasiyofaa katika jamii, mila hiyo ikiwepo lazima ipigwe vita.
Monday, January 5, 2015


Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akionyesha picha za viongozi wa Panya Road kwa wanahabari.
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,
linawashikilia watu 510 wakiwemo viongozi watatu wa kundi
linalojihusisha na uhalifu la ‘Panya Road’ .Watu hao wamekamatwa katika operesheni inayoendeshwa na jeshi hilo, kupambana na uhalifu.
Subscribe to:
Posts (Atom)