
MAAJABU! Ndivyo unavyoweza kusema unapokutana na mwanaume mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Frank Kalamu (53) mkazi wa Ilala Jijini Dar es Salaam, aliyetoa ushuhuda wa kufunga mwaka kwamba kwa zaidi ya miaka miwili, alikuwa akipata siku zake kama ilivyo kwa wanawake, ingawa yeye ni kupitia njia ya haja kubwa.

Akizungumza na waandishi wetu nje ya kanisa, Frank alisema awali alikuwa mzima lakini ghafla alianza kwa kukosa hamu ya kushiriki tendo na mkewe, ingawa alipojaribu kuchepuka, alimudu vyema kazi hiyo.
“Baadaye dalili zilizidi kuongezeka, nikajikuta nikipata maumivu chini ya kitovu na kuanza kutoka damu kila mwezi hasa nikiwa najisaidia haja kubwa, hali hiyo huambatana na kutoka nyama sehemu za haja kubwa.

Baada ya kuona anamaliza fedha bila kupata nafuu, Frank aliamua kutafuta huduma ya kiroho ambapo akiwa kanisani hapo, Nabii Yaspi alimwambia kuwa alikuwa amerogwa na mtu aliyemtaja kwa jina la Saidi, ambaye mgonjwa huyo alimtambua kama rafiki yake wa zamani aliyewahi kumhisi kuwa alitembea na mchumba wake.

0 comments:
Post a Comment